GAZETI LA UCHAMBUZI MAKINI LENYE KUIHUSU NA KUIGUSA JAMII. NI GAZETI LA KILA WIKI. LITAANZA KUONEKANA MITAANI JUMANNE, MACHI 31, 2009. USIKOSE NAKALA YAKO!
Friday, February 08, 2008
Hotuba Ya Lowassa Jana Bungeni

"Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kuchukua nafasi hii kukushukuru sana kwa kunifanya msemaji wa kwanza katika hoja hii.

Lakini la pili, nimpongeze Dk. Harrison Mkwakyembe, Mwenyekiti wa kamati Teule kwa kuwasilisha kwa mbwembwe nyingi sana taarifa yake, mbwembwe zilikuwa nzuri kweli.


Kwa kazi nzuri kwa maoni yao, wamewasilisha vizuri. Lakini nimesimama kuweka kwenye kumbukumbu kutoridhika kwangu na jinsi kazi hiyo ilivyofanywa. Mheshimiwa Dk. Mwakyembe ni Mwanasheria, tena Daktari alikuwa anafundisha Chuo Kikuu. Moja ya vitu alivyokuwa anafundisha ni "Natural Justice".
Mheshimiwa Spika, wewe ni Mwanasheria unafahamu suala la Natural Justice. Kwamba Kamati Teule imesikiliza watu wengine wote pamoja na wanaoita minong'ono ya mitaani, wamesafiri mpaka Marekani kutafuta mashahidi, lakini mimi ambaye ni mmoja kati ya watuhumiwa mle hawakunihoji hata siku moja.
Mheshimiwa Spika, nimesimama kueleza masikitiko yangu. Ofisi ya Bunge mpaka ofisini kwangu hata kama wangeniita ningekwenda kwa miguu kama hamna gari na nilikuwa tayari kufanya hivyo.

Hawa ni watu makini sana siwezi kuamini kwamba wanaweza wakafanya oversite kama hiyo. Kwa sababu katika kila hoja walizojenga wamesema Waziri Mkuu ilikuwa hivi. Kulikuwa na shida gani kuja kuniuliza Waziri Mkuu wanasema uliotoa dokezo hili ni sawa sawa kweli? Kulikuwa na shida gani kwa mfano kufuata utaratibu wa Westminster kuthibitisha hapo unaposema mwenye Richmond ni fulani uka-lay on the table records na ushahidi kuwa ni fulani.

Mheshimiwa Spika, Taifa letu ni Taifa changa, lakini chombo hiki ndiyo mahali pa demokrasia pakubwa katika nchi pote, hapa ndipo penyewe. Kama katika chombo hiki haki haitaonekana kutendeka nchi yetu haitakwenda vizuri. Hapa ndipo tunategemea tuwaonyeshe umakini wetu, umahiri wetu katika mambo ya demokrasia. Kwa nhiyo nilichofanyiwa napenda kuweka kumbukumbu sawa kwamba naona si sahihi, nimefadhaika sana, nimedhalilishwa sana, nimeonewa sana katika hili.
Maana zimechukuliwa tuhuma zikaelezwa hapa kwamba hivi ndivyo ilivyo. Mimi sijauliza. Kulikuwa na shida gani kuniuliza, kwa nini muamini minong'ono ya mitaani kuliko maelezo yangu. Sisi wote hapa ni wanasiasa tukianza kuamini minong'ono ya mitaani niambieni mwanasiasa atakayesimama. Hatuwezi, Tume imepewa muda wa kutosha lakini inashindwa kumuona mtu ambaye wanamtuhumu na wanamsema kwa kirefu sana.

Mheshimiwa Spika, lakini hata pale uliponinong'oneza ukaniambia una ushahidi wowote? Nilikupa ushahidi huo wa maandishi. Katika taarifa yao hakuna hata moja ya ushahidi ambao umetoka Waziri Mkuu. Kile kitabu cha majedwali kimejaa majedwali mengi pamoja na magazeti mpaka ya Udaku lakini maelezo ya Waziri Mkuu hakuna hata moja.

Mheshimiwa Spika, naamini ingekuwa ni heshima wangeiweka halafu wakasema tunakataa kitambulisho hiki kwa sababu hii na hii, hiyo ndiyo imejengwa hoja. Lakini kujenga hoja na kuja hapa Bungeni tunahutubia nchi nzima na kusema Waziri Mkuu amefanya hiki, amefanya hiki bila ya kumsikiliza nachelea kuuliza hivi mtu wa chini itakuwaje?

Mheshimiwa Spika, lakini nimetafakari kwa makini sana jambo hili nikajiuliza hivi kulikoni mpaka watu wazima wenye uwezo wao, watu maarufu wenye heshima zao, mpaka wafike mahali waache jambo la msingi kama hilo kulikoni? Mimi nadhani there is a wish which I am going to grant, ni Uwaziri Mkuu. Nadhani tatizo ni Uwaziri Mkuu. Kwamba ionekane Waziri Mkuu ndio amefanya haya, tumuondolee heshima au tumwajibishe.

Mheshimiwa Spika, nimetafakari kwa niaba ya chama changu, kwa niaba ya Serikali yangu nimeamua kumwandikia Rais barua ya kumwomba niachie ngazi. Nafanya hivyo kwa moyo mweupe kabisa ili kuonyesha dhana ya uwajibikaji lakini kutokubaliana na utaratibu uliotumika kusema uongo ndani ya Bunge wa kumsingizia mtu.

Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii kumshukuru sana Rais kwa heshima aliyonipa ya kutumikia nchi hii kwa Uwaziri Mkuu kwa miaka miwili.
Namshukuru sana Mheshimiwa Rais.

Nakushukuru wewe, nawashukuru Mawaziri na Manaibu Waziri, nawshukuru Waheshimiwa Wabunge na wanachama wa CCM tuliyosimamia Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo nashukuru".
 
©Maggid | Date:8.2.08 | Permalink| | Send To Your Friend |


Comment: 11


  • Date: Fri Feb 08, 09:06:00 AM EAT, Anonymous Mliakuvana

    The Prime Minister has a point! Why wasn't he asked about these allegations wakati wa uchunguzi wa Kamati Teule?

    Je, inawezekana kuwa waziri mkuu alivyoambiwa na wizara ya Nishati na Madini kuwa wamechagua Richmond ilete umeme wa dharura na yeye waziri mkuu akawahamasisha wafanye chap chap kusign mkataba? Manaake yeye hakuchagua hawa Richmond na pengine alikuwa anaeelewa kwamba watu wote husika i.e. wizara, ofisi za mwana sheria mkuu, TANESCO etc wamefanya kazi yao ipasavyo.

    Just wondering aloud........

     
  • Date: Fri Feb 08, 11:17:00 AM EAT, Anonymous Phatlorenzo

    Simple answer: Kwa nini Lowassa aliitisha vikao vya usiku akiwatisha mawaziri na manaibu wao siku ya Jumatano usiku ili wautetee uamuzi wa Serikali na kuikataa hiyo ripoti?
    Kama yeye ni safi kwa nini alikuwa anatapatapa?

     
  • Date: Fri Feb 08, 11:22:00 AM EAT, Anonymous Phatlorenzo

    Milango ya Kamati ilikuwa wazi kwa mwananchi yeyote yule ambaye alikuwa na taarifa yeyote kuhusu RICHMONDULI GATE kuwasilisha taarifa hiyo mbele ya Kamati ya Mwakyembe. Waziri Mkuu kama Kiongozi mkuu Serikalini na kwa kuzingatia ushiriki wake wa karibu katika suala hilo, ilitarajiwa awe mtu wa kwanza kutoa taarifa ama maelezo juu ya mchakato wote wa utoaji wa tender hiyo mbele ya Tume. Kwa ujeuri na kiburi chake alijua tume haitathubutu kuhusisha mambo yanayomhusu yeye kwenye taarifa yao. Alijua wazi kulikuwa na mawasiliano ya moja kwa moja kati ya ofisi yake na ofisi ya wizara ya nishati na madini na hilo lingemsukuma kwenda mbele ya tume kueleza kile alichokuwa anakifahamu, hakufanya hivyo na sasa anamlalamikia Dr. Mwakyembe kuwa ripoti ameiwasilisha kwa mbwembwe, hii sio hoja kwa sasa. La msingi ni kuwa ni kweli aliweka shinikizo la utoaji wa tender hiyo kwa ujeuri na nguvu zake binafsi.

     
  • Date: Fri Feb 08, 11:50:00 AM EAT, Anonymous Anonymous

    Mwizi ni mwizi au FISADI wanatakiwa wapelekwe Ukonga wakae huko wakati uchunguzi unafanywa,AIBU TUPU wazi mkuu mzima anatetea ufisadi.

     
  • Date: Fri Feb 08, 12:12:00 PM EAT, Anonymous Anonymous

    Simtetei Lowasa lakini kama mtu ambaye niko nje ya ulingo naangalia kinachoendelea bila ushabiki maswali ya Lowasa yanaonyesha pamoja na ufisadi kuna kitu zaidi ya hicho wanachogombania, ukizingatia Mwakyembe ni best wa Mwandosya, lakini pamoja na hayo, kwanini kamati haikumuita na kumuuliza ikapata upande wake wa story?
    Sasa ameondoka huku ameacha maswali mengi kuliko majibu. Kwa waliokwenda jeshini enzi hizo JKT unakumbuka ukitaka kusave noma unasema tu nimetumwa na afande. Sasa afande akiwa wa level ya chini hawezi kwenda kumuuliza afande uliyemtaja ambaye yuko ngazi ya juu. Kuna siku ukweli mzima utajulikana kama hadithi ya Iddi Simba na sukari. Kosa liko kwa Msabaha kwanini hakufuata maamuzi ya baraza la mawaziri. Nayeye PM kosa lake ni uzembe wa kuamini kila alichokuwa akiambiwa na Msabaha. Mkumbuke huyo anayesemwa Mohamed Salehe ni mume mwenza wa Msabaha, inawezekana ngoma ilikuwa yao wao peke yao akaamua kumpa habari anazozitaka yeye huyo PM ili atimize matakwa yake wakati wa kuanguka mtu anasema lazima nidondoke na mtu siwezi kuondoka peke yangu.

    I give Lowassa benefit of doubt until proven guilty with evidences, not just hearsay ambayo watu walikataa kuisema katika kiapo. They should have indicted him kwenye kiapo na si nje ya kiapo kama walivyofanya Kazaura na Msabaha. Kwanini walinong'ona hizo tuhuma zao nje ya kiapo? Guys politicis is a dirty game anyone can play it the way it favours him they all have motives behind. Ingekuwa ripoti hii imeandikwa na third party ningeamini yoote 100%.

    One thing for sure, Mwandosya will never be a PM (he is very arrogant), Mwakyembe will never get any Ministrial post, Anne Kilango (she is bitter because her husband is no longer Makamu wa Mwenyekiti) will not get any Ministerial post. And JK will continue to travel outside the country because that is part of his TOR as a President of the country, he invite and get invited with other presidents.

     
  • Date: Fri Feb 08, 12:30:00 PM EAT, Anonymous Anonymous

    Fisadi namba moja huyo.kwanza RICHMOND Kirefu chake ni RICHAD MONDOLI mtoto wa huyo fisadi

     
  • Date: Fri Feb 08, 02:00:00 PM EAT, Anonymous mtoto wa mkulima

    Anonymous wa 8/2/08 12:30 PM usidangaye umma, wewe ni mtetezi wa Lowasa moja kwa moja, taarifa ya kamati imeonyesha na ushahidi usio shaka kwa kila hoja, kikubwa ni kiburi cha mafisadi huyo nduguyo aliamini kuwa hatokuswa na kamati ingefanya kama ilivyokuwa ikifanyika huko nyuma lakini akasahau kuwa hiki ni kizazi kingine, subiri ya bot itoke ambako hakuitwa lakini tayari imevuja kuwa naye katajwa.

    suala la Mwandosya halina msingi hapa, yeye ndiye alikuwa bingwa wa kuwachafua wenzie akiwemo huyo mwandisya kwa kuwatumia waandishi wa habari.

    Lowasa hana haja ya kutafuta mchawi ni yeye mwenyewe, na hiyo kamati wala asiitole macho kwani mazingira yanaonyesha wazi ushiriki mshikaji- JK, eg hotuba yake ya mwisho wa mwezi na kule pemba kuhusu viongozi zimetokana na maudhui yaliyomo kwenye taarifa hiyo ikiwa na maana kwamba kama alizungumzia suala hilo kabla ya bunge ni wazi alikuwa na feedback ya uchunguzi, muda ilosomwa na yeye mwenyewe siku hiyo hiyo kutua dodoma inaonyesha wazi alifahamu nini bomu hilo likokuwa likielekea.

    kamati haikuundwa na Dr Mwakyembe pekee, ilikuwa na wajumbe wenye misimamo kama Manyanya na Selelii.

    leo analalamika kutotendewa haki, amesahau alivyokuwa akiwadhalilisha viongozi wa chini ya kwenye mikutano ya hadhara kwa kjuwatwisha tuhuma huku yeye akiweka mbali.

    Watanzania tuache unafiki, tuambiane ukweli, huyo bwana ni fisadi namba moja, lakini katika yote lazima tuelewe kuwa MZIMU WA MZEE WA KIZANAKI-JULIUS umeanza kuwatafuna mafisadi na huyo alimwambia wazi kuwa hafai akang'ang'ania.

     
  • Date: Fri Feb 08, 02:07:00 PM EAT, Anonymous Anonymous

    Kamwangusha marehemu Sokoine,Mmasai mwenzie mfano wa kuigwa na kila Masai kwa kufanya kazi usiku na mchana kutetea wanyonge wa nchi hii.

    Kumbe wamasai wako wengi na wa aina tofauti ndio sasa nimejua.Nilikuwa nafikiri wote wako kama Sokoine.

     
  • Date: Fri Feb 08, 02:54:00 PM EAT, Anonymous anon

    Lowassa(Richmond) hakuwa na ushaidi wowote wa maana,alichotaka ni wamuite hili atumie mwanya huo kuwatisha ,kuwahonga,kuwarubuni.
    mbona business partner wake Rostam Aziz(Dorwan)na Daniel yona wamekataa kuhojiwa.

    nadhani hakuna haja ya kumsikiliza ndg lowassa kwani ni fisadi sisi watanzania hivi sasa tunanunua unitmoja ya umeme kwa shilingi 158 toka kwenye shilingi 40 tulizo kuwa tunanunua mwaka jana kumbe pesa hizi zote tunawapa wakina lowassa na Richmond yake(soma ripoti ya mwakyembe?
    sasa asikilizwe hili harudishe hizo pesa au?
    let him go....he can go to hell!

     
  • Date: Fri Feb 08, 05:53:00 PM EAT, Anonymous Advocate Jasha

    Ndugu Lowassa hakutegemea hilo lilotokea kwani imekua kawaida kwa ka utawala uliopo kila inapotokea kashfa za ufisadi ujaribu kuzifukia kwa kwa kuunda kamati za uchunguzi au kupitia Takukuru au mwanasheria mkuu vyombo hivi vimekua kama taasisi za kuwalinda MAFISADI badala ya kulinda masilahi ya wananchi.Kutokana na shinikizo la wapinzani,wananchi,wafadhili na wabunge wengi wa CCM kuona chama chao kinaelekea ukingoni na kutumiwa na wajanja wachache kutimiza ufisandi wao this time mazingaombwe hayo sasa yamegonga mwamba.Nd.Lowassa ,Rais,Spika baaada ya kuipata taarifa hiyo na kugundua kua ni vitu vya kweli wakaanza kufanya jitiahada zote kuizima lakini kutokana na mazingira niliyo yataja hapo juu ilishindikana hivyo kujikuta ana kwa ana na ukweli.Hotuba yake kabla ya kujiuzulu naifananisha na maneno ya mtapa maji .Uongo,sikuitwa na kamati ,kunamkono wa mtu n.kSawa ukuitwa na kamati kutoa maelezo,kwanini ukutumia muda huo katika hotuba yako ya kujiuzulu katika bunge kuiumbua kamati kwa kusema ukweli na uongo ni upi?Hii naifananisha na mtu aliyefumaniwa akitembea na mke wa mtu kwa vile akulitegemea kauli inayozunguka ulimini ni waongo,sio kweli.Bwana we uko uchi mke wa mtu yuko uchi ndani ya nyumba ya kulala wageni ulikua unafanya nini ?upi uongo?Badala yake ndg.Lowassa anatoa hotuba zisizokua wala kichwa wala miguu.Huyu ndg kwanza anabidi aseme uongo ni upi katika taarifa hiyo na athibitishe .Kama atathibitisha hivyo basi kamati ichuliwe hatua na kama atashindwa kufanya hivyo basi Spika amburuze mahakamani kwa kulikashifu bunge.y
    Yafuatayo ni ushauri wangu kwa Mh.Rais kama kweli amepania kupambana na ufisadi na rushwa;
    1.Washukiwa wote wanapaswa kukamatwa mara moja,akaunt na mali zao kuzuiwa wakati mkondo wa sheria ukichukua nafasi yake.Kwanini?Nafafanua kwanza ili wasikimbia au kuingilia au kuaribu ushahidi,Pili ni kwa ajiri ya usalama wao pamoja na mali zaokwani chuki ya Wananchi kwa mafisadi imefikia kiwango kikubwa katika hali hiyo kua kwao huru na mali zao kutolindwa na serikali ni hatari kwao.
    2.Viongozi wa Takukuru na mwanasheria mkuu wawajibishe mara moja.
    3.Bunge livunjjwe na kutangaza uchaguzi mara moja ili wabunge wakapime imani zao kwa wananchi kwani bunge ili la CCM limechangia kwa kiasi kikubwa kufikia katika hali hii tuliyofikia bunge lisilolinda masilahi ya walala hoi bali masilahi yao wabunge ukiondoa wapinzani hambao ndio wameibua kashfa zote za ufisadi.
    4.Uundaji wa baraza la mawaziri usifate itikadi za kichama bali sifa na uwezo wa mtu .
    5.Watuhumiwa wate pindi mkondo wa sheria utakapogundua kuwa wakosaji walipe gharama zote zilizotumika kuchunguza uozo huo.
    5.Kujiuzulu sio wakati wote nia adhabu,kitendo cha busara au ushujaa.Kama waziri wa mambo ya ndani na miundo mbinu akijiuzulu kufuatia ajari zinazotekea na kupotza maisha ya watu kila siku ambapo mambo mengi yako nje ya uwezo wake kitendo hiki tunaweza kukiita cha kishujaa na cha busara na kumpa Mh.Rais nafasi ya kutafuta mchakato wa kuimarisha sekta hiyo.Lakini kama waziri mkuu,waziri au kiongozi yeyote atakapochota pesa za walalahoi kwa ufisadi na rushwa na kujiuzulu na kwenda kutumia pesa zake kwa njia ya ufisadi huyu sio shujaa ni fisadi na mahala pake ni gerezani.Kwani kumekua kunawatu wanaosema hatua ya kujiuzulu ni za kishujaa na za busara ni ushujaa gain aliofanya ndg.Lowassa kuwabebesha wananchi gharama za umeme zisizo na msingi?Anaweza kua Shujaa mbele ya Richimud lakini mbele ya walala hoi ni FISADI.
    Hatua nilizozitaja hapo juu ziwe kwa viongozi wote kwa kufanya hivo, ile kauli ambayo imesahalikakaUONGOZI NI DHAMANA.Mh.Rais kama hayo niliyoyataja hayatatekelezwa .Yotea hayo yatakua mazingaombwe na hatutasita kukushirikisha na yote yanayotokea na tutachukulia kujiuzulu kwa Lowassa ni mbuzi wa kafara.MUNGU IBARIKI TANZANIA.

     
  • Date: Mon Feb 11, 02:17:00 PM EAT, Anonymous Anonymous

    Naona sasa vumbi limetulia kidogo hebu tumwone EL na nia njema ya serikali. Nia njema ilikuwa kupunguza makali ya mgao wa umeme ambao safari uliathiri hata viwanda vikubwa hivyo kuvuruga uchumi wa nchi.Kwa hili hakuna ubishi. Kama waziri mkuu alitakiwa kujua jinsi IPTL walivyotumia mgao wa umeme uliopita kupitisha mkataba mbovu ambao, kama ule wa Gauss na chessboard,unatugharimu wananchi pesa nyingi.Kinyume chake umakini haukutumika katika uteuzi na pia kuthibitisha uwezo wa Richmond. Kwa kutofanya hivyo ni lazima akubali kuwajibika, kwani si hekima kiongozi kuwasikiliza(100%) sana wasaidizi wake na kuwapa nguvu ya kushinikiza maamuzi. Je anataka tuamini alichomekewa na akina Msabaha na Mume mwenzie aliyekuwa akidouble deal? Kimsingi EL hana sababu ya kulalamika maandishi yalishaandikwa ukutani alipaswa kuyasoma badala ya kuwapa TUKUKURU_ndogondogo ambao uzoefu wao ni kunasa mahakimu. Hapo alikuwa na nafasi ya kuspin to his adavantage. Wakati ukuta yamemkuta.

     
   
 
Copyright 2006 © MAGGID MJENGWA. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu