Binti wa Mzee Chrisant Mzindakaya. Naye ameshinda U- NEC. Violet ni Mtangazaji wa redio ya Chama, redio Uhuru.
Binti wa Mzee Chrisant Mzindakaya. Naye ameshinda U- NEC. Violet ni Mtangazaji wa redio ya Chama, redio Uhuru.Date: Tue Nov 06, 11:50:00 AM EAT,
Date: Tue Nov 06, 12:29:00 PM EAT,
Date: Tue Nov 06, 02:37:00 PM EAT,
Date: Tue Nov 06, 04:22:00 PM EAT,
Zawadi Kawawa,Nape Nnauye,Violet Mzindakaya,Rizwaini Kiwete, Benno Malisa.
Hivi ni aibu gani jamani hii yaani mmeshindwa kuficha uozo wenu mpaka mnampitisha hata Benno Malisa??
Nomba ikumbukwe kuwa Rizwani na Benno ni marafiki wakubwa sana na wamesoma wote Chuo kikuu cha Dar es salaam, dogo kapewa chance ya kuwa makamu mwenyekiti wa umoja wa vijana wa ccm, kumbuka Benno ni fress from school hajui lolote kwenye siasa, lakini kapachikwa na sasa ndo huyoo kaingia kwenye Nec haya 2010 utasikia ni Mbunge na usishangae ukaambiwa Benno ni waziri au Naibu waziri. doh
any way tutafika tu
Date: Tue Nov 06, 05:30:00 PM EAT,
Naunga mkono alichosema Msekwa.Ni vizuri Chama kianze kuajiri au kuchukua watoto wenye akili sana toka vyuo vikuu ndani ndani na nje ya nchi na kuwa-groom kwenye chama.Vinginevyo nchi itaishia tu kuongozwa na watoto wa viongozi na makada tu karne na karne ambao sina uhakika kama wengi wao IQ yao iko juu sana na kama wana stamina za kutosha kuhimili mikikimikiki ya mapambano ya pinzani kali na changamoto kali za kisiasa kwa hoja kali za upeo mkubwa wa juu sana.Sina uhakika
Naona Chama kama CHADEMA kimeanza kulenga wasomi wenye upeo na kuwagroom,CCM ikiendekeza watoto wa vigogo isishangae kukaukiwa hoja mbeleni na kutafuta maji ya kunywa kwa kukosa cha kujibu.
CCM iskilize ushauri wa MSEKWA.Anzeni kutafuta watu wenye akili hasa toka vyuoni waingie na muwape nafasi ndani ya chama.
Kama hawataki kugombea nafasi wekeni nafasi za wajumbe wa kuteuliwa.Wateueni wapeni madaraka waingizeni hadi NEC kwa kuteuliwa ikibidi.Sababu katika siasa watu wazuri mara ingine huwa hawapendi kugombea kwa kura lakini ukiwateua ukawaingiza utawaona ubora wao.
Ushindi huu nautazama kwa jicho tofauti mfano kundi la vijana walioingia NEC washindi wengi wanatoka Dar es salaam,wilaya ya Kinondoni sijui ni bahati mbaya au ni nini ? Na wengi walioteuliwa kugombea katika kundi hili pia walitoka wilaya ya Kinondoni!!!! Kimshikamano kitaifa ni sawa kuteua wengi toka wilaya moja tu kugombea kwenye chombo kikuu kama NEC????
Wataalamu wa tafiti za kisiasa mnaweza saidia hili!
koloboi@yahoo.com
Date: Tue Nov 06, 10:28:00 PM EAT,
Date: Wed Nov 07, 04:21:00 PM EAT,
naona mzee mzindakaya amerithisha mikoba kwa huyu binti wake!
basi atasota na uNEC wake mpaka azeeke kama dad!ndiyo CCM ilivyo!