


Nilipokuwa Sweden miezi kadhaa iliyopita nilikutana na Msweden mpenzi wa kandanda. Aliangalia picha za vijana hao wa Gangilona Kids na akaona wanahitaji msaada wa vifaa vya michezo. Kama mchezo, aliahidi angenitumia kwa posta. Juzi hapa vimefika; jezi seti mbili, mipira sita, viatu kwa wachezaji kumi na nne na simu ya mkononi ya kocha.Vyote hivyo ni kwa timu ya watoto chini ya umri wa miaka 12. Thamani ya vifaa hivyo ni karibu shilingi za Kitanzania milioni moja na nusu. Pichani ni jana mchana wakati nikikabidhi vifaa hivyo kwa kocha wa timu hiyo Rashid Zongo na nahodha Immanuel Shoo.
I see Mzee Mjengwa kampeni zako za ubunge ndio zimeanza tena!!
tunahitaji watu kama wewe bungeni....