GAZETI LA UCHAMBUZI MAKINI LENYE KUIHUSU NA KUIGUSA JAMII. NI GAZETI LA KILA WIKI. LITAANZA KUONEKANA MITAANI JUMANNE, MACHI 31, 2009. USIKOSE NAKALA YAKO!
Sunday, July 05, 2009
Precision Air


Precision Air yazindua safari ya Mwanza - Nairobi

Jumapili, Julai 5, 2009:

SHIRIKA la ndege la Precision Air limezindua safari ya moja kwa moja ya kutoka Mwanza, Tanzania kwenda Nairobi, Kenya.

Uzinduzi huo uliofanyika mwishoni mwa wiki jijini Mwanza, unafanya Precision Air kuwa na safari za moja kwa moja 13 katika huduma zinazotolewa na shirika hilo Afrika Mashariki, na safari 381 zinazofanywa na ndege za shirika hilo kwa wiki, hivyo kuzidi kupanuka kwa mtandao wake Tanzania.

Katika kuzindua safari hiyo, baadhi ya abiria na wadau wa Precision Air, walisafiri kutoka Nairobi na kutua Mwanza walikolakiwa na baadhi ya maofisa wa Precision Air, wakiwamo Meneja wa Precision Air Kanda ya Ziwa, Cecilia Odemba, Ofisa Mawasiliano wa Precision Air, Mabhe Matinyi na Ofisa wa Ratiba na Mipango ya Mtandao wa Precision Air, Patrick Mwakasungula.

Pia wasafiri hao wakiwamo waandishi wa habari na wadau wengine wa sekta ya usafiri wa anga, walilakiwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza, Leonard Bihondo kabla ya kutembelea maeneo mbalimbali ya Jiji la Mwanza.

Safari hiyo kati ya Nairobi na Mwanza, kwa kiasi kikubwa itarahisisha usafiri kati ya miji hiyo na itafupisha muda wa safari kuwa saa 1 na dakika 20 tu ikilinganishwa na saa 2 na dakika 45 iwapo ndege itapitia Kilimanjaro.

Safari hizo za moja kwa moja kutoka Mwanza kwenda Nairobi na kutoka Nairobi kwenda Mwanza, zitakuwa zikifanyika mara nane kwa wiki. Awali, shirika hilo la ndege Ð ambalo asilimia 49 inamilikiwa na Shirika la Ndege la Kenya (Kenya Airways) Ð lilikuwa likifanya safari mara nne kwa wiki kutoka Mwanza kupitia Kilimanjaro.

ÒSafari ya moja kwa moja kwenda Mwanza itawarahisishia abiria usafiri. Pia itaboresha usafiri wa kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) kwenda Afrika Kusini, Dubai, London, Entebbe na Doha,Ó alisema Alfonce Kioko, Mkurugenzi Mkuu wa Precision Air.

Alisema shirika hilo limewekeza katika safari hiyo ya Mwanza ili kuwarahisishia wateja usafiri na kuwalenga zaidi wafanyabiashara wa samaki na bidhaa nyinginezo jijini Mwanza.
Kioko alisema abiria wengi katika njia hiyo ni wasafiri kati ya Mwanza na Nairobi na pia kuna abiria wengine wanaohitaji kwenda JKIA ili kuunganisha ndege nyingine.

ÒIdadi ya abiria wanaosafiri na ndege za Precision Air imeongezeka kutoka 216,990 kwa mwaka 2004 hadi 538,305 mwaka huu,Ó alisema Kioko.

Precision Air hivi sasa inafanya safari zake katika mikoa 13 nchini na ina mpango wa kupanua wigo kwa kufanya safari za kimataifa katika miji ya Luanda, Lubumbashi, Johannesburg, Harare, Pemba na Nampula, Msumbiji, Lilongwe na Hahaya, ikiwa ni sehemu ya kujiimarisha zaidi.

Pia, katika kuboresha safari za ndani ya nchi, Precision Air inatarajia kuanzisha safari katika miji ya Mbeya, Songea, Dodoma, Pemba Zanzibar na Tanga.
 
©Maggid | Date:5.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
CCM Uingereza
CHAMA CHA MAPINDUZI
TAWI LA UINGEREZA
MKUTANO MKUU WA TAWI - 26/07/2009 (Jumapili)


Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi Tawi la Uingereza. Mnakaribishwa kwenye Mkutano Mkuu wa Wanachama wote wa Tawi la CCM Uingereza - Jumapili, tarehe 26/07/2009

Anuani: The Warehouse
01 Cumberland Road
Reading
RG1 3LB

Muda: Saa 8 mchana - Saa 12 jioni.

Kutakuwepo na Kadi za CCM ambazo zitatolewa kwa Wanachama wapya (Kadi paundi Tatu - £3, Ada ya mwaka paundi Kumi na Mbili - £12)

Kutakuwa na Chakula, Vinywaji baridi na Viburudisho vingine.


Kwa ufafanuzi zaidi tafadhali wasiliana na Katibu wa Tawi;
Susan Mzee kwenye barua pepe: ccmlondon@gmail.com

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI



Susan Mzee
Katibu wa Tawi
CCM - Uingereza
www.ccmlondonuk.org
 
©Maggid | Date:5.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Hii Imekaaje?


Ahsante ya picha kwa mwenzetu Shamsa Salim Ahmed Salim.
 
©Maggid | Date:5.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 3
Saturday, July 04, 2009
Shaaban Dede



Mratibu wa bendi ya DDC Mlimani Park , Juma Mbizo (mwenye miwani) akiwa na nyota wa bendi hiyo , Shaaban Dede . Hiyo ilikuwa jana nyumbani kwa Juma Mbizo maeneo ya Magomeni Kagera , jijini Dar es Salaam . Imeletwa na mdau wa http://www.kwanzajamii.com
 
©Maggid | Date:4.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
BBC Dira Ya Dunia Kuzinduliwa Na Vinjonjo!



Dira ya Dunia kuzinduliwa na vionjo vipya


London, 3 Julai 2009. Wasikilizaji wa matangazo ya Dira ya Dunia yenye kuleta taarifa, makala na uchambuzi, wajiandae kwa mshangao wa kuridhika watakaposikiliza redio zao Jumatatu ya tarehe 6 Julai 2009.



Matangazo hayo yenye wasikilizaji wengi zaidi katika Idhaa ya Kiswahili ya BBC, yamesukwa upya kwa kunogeshwa na muziki mpya, vibwagizo na mtindo mpya wa usimulizi pamoja na makala na ushirikishaji wa wasikilizaji.



Dira ya Dunia, ambayo sasa itakuwa inasimuliwa na watangazaji wawili kwa wakati mmoja, itaanza kurusha makala maalum ya maswala ya biashara mara mbili kwa wiki na taarifa zaidi za michezo na wachezaji. Matangazo hayo yenye mtizamo mpya yatakuwa yakirusha taarifa zenye uchambuzi kutoka kwa waandishi na wataalam wa fani mbali mbali, pia kushirikisha wasikilizaji wa SMS na kutoa maoni kwa njia ya simu.



Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC - ambaye pia ni mmoja wa watangazaji wa Dira ya Dunia - Solomon Mugera anafafanua: “Dira ya Dunia mpya itatumia mtindo wa uchangamfu na vishindo; makala ya Biashara imetokana na shindalo la kutafuta kijana mwenye kipaji cha biashara, Faidika na BBC. Wasikilizaji walitaka kupata jukwaa la kubadilishana mbinu, mawazo, uzoefu na ushauri, na tulidhani Dira ingekuwa matangazo muafaka kufanya hivyo.”



Pamoja na Solomon Mugera, watangazaji wengine wa Dira ni Charles Hilary, Suluma Kassim, Salim Kikeke, Hassan Mhelela, Alex Mureithi, Peter Musembi, Flora Nducha, Mariam Omar, Ali Saleh, Idd Seif na Zuhura Yunus.

Mabadiliko haya ya Dira ya Dunia ni mwanzo tu wa mageuzi makubwa ya vipindi vya Idhaa ya Kiswahili ya BBC, Solomon Mugera anaeleza: “Hivi karibuni tutafanya mabadiliko kwenye vipindi vyetu vyote ikiwa ni pamoja na matangazo yetu ya alfajiri, Amka na BBC, na pia taarifa zetu za habari ambazo hurushwa kila baada ya saa moja.”



Matangazo ya Dira ya Dunia, yenye urefu wa saa moja, husikika kuanzia saa kumi na mbili na nusu jioni kwa majira ya Afrika Mashariki.Makala maalum kama Uchumi kila Ijumaa, inayotoa taarifa za uchumi kutoka ndani na nje ya Afrika Mashariki na Kati, na makala ya TeknoMaarifa kila Jumanne ambayo hurusha habari za sayansi na teknolojia.







Kwa Maelezo zaidi tafadhali wasiliana na:



BBC World Service Publicity

+44 207 557 2944; wspublicity@bbc.co.uk
 
©Maggid | Date:4.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Friday, July 03, 2009
Subi Sabato Anaelimisha!


Juma la jana pale Ubungo nilimkuta bwana huyu ( pichani) akiwa amezama kwenye makala ya Subi kuhusiana na matibabu ya kisukari. Makala hiyo ilichapwa kwenye KWANZA JAMII toleo lililopita. Nilimwuliza bwana yule kuhusiana na mada hiyo. Akanijibu; kwake anafuatilia mada hizo kila Jumanne inapotoka KJ. Anasema Kisukari ni ugonjwa wa kifamilia. Mwanafamilia mmoja akiugua kisukari,basi,kwa namna moja au nyingine wote mnajikuta mkihusika na mgonjwa huyo kuanzia chakula na mengineyo. Hii ni tofauti na malaria, aliniambia bwana yule pale Ubungo.
 
©Maggid | Date:3.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
Ukitaka Kujua Keshokutwa Ya Nchi Itakuwaje...



Angalia hali za watoto wa nchi kwa leo hii.
 
©Maggid | Date:3.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
Ombwe ( Vacuum)


Chalinze,leo alasiri.
 
©Maggid | Date:3.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 2
Wa Kujipakulia!


Kobic Restaurant,Chalinze,leo alasiri. Nilisimama na kupata mlo mahali hapo nikitokea Iringa. Nimewasili Kinondoni Biafra jioni ya leo.
 
©Maggid | Date:3.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Mama Salma Kikwete Asisitiza....


Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiingia katika ukumbi wa mikutano wa Sirte tayari kuhudhuria kikao maalumu cha kamati ya Umoja wa Wake wa Marais wa Afrika dhidi ya Ukimwi OAFLA, mjini Sirte Libya(picha na Freddy Maro)


MAMA SALMA KIKWETE ASISITIZA KUUNDWA KWA SEKRETARIETI YA KUDUMU YA OAFLA.

Na Freddy Maro, Sirte, Libya

3 Julai,2009.



Mke wa Rais Mama Salma Kikwete ametoa wito wa kimarisha zaidi umoja wa Wake wa Marais wa Afrika dhidi ya gonjwa la ukimwi(Organisation of African First Ladies Against AIDS (OAFLA )kwa kuanzisha ofisi za kanda na kuwa na sekretarieti ya kudumu itakayokuwa na wafanyakazi wenye ajira ya kudumu.



Akizungumza wakati wa mkutano maalumu wa kamati ya umoja huo wa OAFLA mjini Sirte Libya Mama Kikwete alisema kuwa lengo kuu la kuundwa kwa sekretarieti lilikuwa ni kuimarisha sekretarieti za nchi wanachama.



“Ninasharuri kuwa utaratibu wa kuimarisha Taasisi ya OAFLA upewe kipaumbele na mkakati madhubuti.Kama tuataendelea kuwa na Sekretarieti inayozunguka,basi tufanye iwe imara zaidi.Mbinu rahisi zaidi ni kuwezesha kuwa na ofisi za kudumu za kanda na kuweka mkazo wa kuhakikisha kuwa ofisi hizi zinawaunganisha na kuwakutanisha wanachama mara kwa mara”, alisema Mama Kikwete ambaye aliungwa mkono na wajumbe wote wa mkutano huo.



Mama Kikwete aliendelea kusisitiza kuwa pendekezo las kuundwa kwa sekretarieti ya kudumu lililotolewa katika vikao vya awali vya OAFLA na wataalamu waliofanya tathmini juu ya uendeshaji wa taasisi hiyo, ni vyema likatekelezwa mapema ili kuiwezesha OAFLA kuwa na ufanisi zaidi katika kutekeleza malengo yake.



Mke wa Rais aliwakumbusha wanachama wenzake kuwa mwezi Februari mwaka huu walikubaliana kuwa ofisi za kanda zipewe dola elfu ishirini ili ziweze kujiimarisha na kupendekeza kuwa ofisi hizo za kanda kwa kushirikiana na UNAIDS na wadau wengine ziandae mikutano ya kanda ili kutoa nafasi kwa wanachama kujifunza kutoka kwa wenzao.



Mama Salma alishauri kuwa kwa kuanzia ni vyema pakawa na ofisa mwajiriwa ndani ya taasisi kiwa sasa na kushirikiana na UNAIDS na wadau wengine ili kazi ya kuunganisha wanachama wa kanda ianze bila kuchelewa akiongeza kuwa ofisi za kanda zitasaidia kuboresha mawasilkiano na sekretarieti kuu ya OAFLA na ofisi za nchi.



Umoja wa Wake wa Marais wa Afrika dhidi ya gonjwa la ukimwi(OAFLA) ilianzishwa kwa lengo la kuwawezesha wake hao wa marais kuunga mkono juhudi za serikali zao katika mapambano dhidi ya ugojwa huo unaoangamiza maisha ya mamilioni ya ya watu Barani Afrika na kuathiri nguvu kazi.



Kikao hicho cha wake wa marais kilifanyika sambamba na mkutano mkuu wa 13 wa Wakuu wa nchi na Serikali za Umoja wa Africa(AU) kilichofanyika katika mji wa Sirte Libya.
 
©Maggid | Date:3.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 2
Thursday, July 02, 2009
JK Na JZ


Kwenye Mkutano wa 13 wa AU, Sirte, Libya. ( Picha: Freddy Maro, Ikulua)
 
©Maggid | Date:2.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Mama Salma Kikwete

Serte, Libya ( Picha: Freddy Maro, Ikulu)
 
©Maggid | Date:2.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 2
Unavyokula Ndivyo Unavyokuwa!


Ukila na kunywa supu ya kichwa cha mbuzi....!
 
©Maggid | Date:2.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 3
Tangawizi
 
©Maggid | Date:2.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Wednesday, July 01, 2009
Inahusu Maarifa!


Pichani kushoto ni Dr. Bukaza Chachage


SUBJECT: INTERNET ACCESS AVAILABILITY
We are glad to inform you that from today you can access internet in our esteemed Tanzania Literature Center (Books 4 Life). The centre is located in the old Neema Crafts workshop at Iringa Retco Building. We offer all basic services associated with internet access.


The Literature Center will be open from 8:30 to 20:30 hours on week days and 8:30-18:30 during weekends.

The cost related to this precious investment is Tshs. 1000 per hour and 500 per half an hour.

We shall appreciate if you will personally come, and/or encourage families, colleagues and friends to utilize our modern, user-friendly internet services.

Be informed also that soon we will bring you a lot of books in various disciplines since we believe books are necessary for our lives. We will definitely keep you posted.


We cordially look forward to seeing you in the Center.


Thanks and welcome,

______________________

Dr. Bukaza Chachage

Entrepreneur

+255 (0)754 074 025

+255 (0)26 2701513
 
©Maggid | Date:1.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
Freddy Macha



SEMINA MBALIMBALI ZA FREDDY MACHA MJINI DAR ES SALAAM, MEI 2009.


Na Mwandishi Maalum



Mwezi Mei mwaka huu mwandishi na mwanamuziki, Freddy Macha aliendesha warsha mbalimbali zilizochangamkiwa na wakazi mjini Dar es Salaam. Warsha zilifanywa ukumbi wa British Council, Soma Cafe (Mikocheni), Shule ya Sekondari Mwandege na Nyumba ya Sanaa na kugawanywa katika mada kuu nne:

1-Uandishi na Fasihi 2- Muziki 3- Maisha Ughaibuni 4- Mazoezi, afya na chakula bora.

Watayarishaji wa shughuli hii ni gazeti jipya la Lucky-Ideas for Living (lililoanzishwa mwaka huu) ambalo linaipa elimu kipa umbele. Akizindua warsha hizo zilizokuwa za bure kwa wananchi, Anna Rugaba, mhariri wa Lucky- alisema lengo kuu la semina ni kutoa fursa kwa baadhi ya watalaamu ndani na nje ya nchi kusaidia maendeleo ya kifikra na kimwili kwa Watanzania.

Kutokana na mvuto ulioonekana baada ya shughuli hiyo iliyochukua siku tano; Lucky imeamua kufanya semina mara kwa mara na wataalamu wenye ujuzi tofauti pale itakapowezekana kigharama. Freddy Macha, anayeishi London na ambaye anajulikana zaidi kama mwanasafu wa magazeti ya Mwananchi, Citizen na Kwanza Jamii anatazamiwa kurudi tena kuendesha semina hizo Septemba mwaka huu.

Kwa habari zaidi na picha, tembelea; http;//www.kitoto.wordpress.com
 
©Maggid | Date:1.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
Untitled


Picha hii niliipiga Jumapili moja hapa Iringa majuma kadhaa yaliyopita. Nyuma anaonekana Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete akisoma.
 
©Maggid | Date:1.7.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 3
Tuesday, June 30, 2009
Nimewasili Iringa Usiku Huu
Safari ya Dar mpaka Iringa siku hizi inachukua zaidi ya saa 10 kutokana na ujenzi wa barabara unaoendelea. Nimefurahi kurudi Iringa yenye baridi.
Maggid
 
©Maggid | Date:30.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
Polisi Wavunja Shughuli Ya Harusi Tanga!


Tukio lisili la kawaida limeripotiwa leo kupitia TBC 1 kwamba polisi mkoani Tanga wameingilia kati na kuvunja shughuli ya harusi kwenye moja ya vijiji vya mkoa huo. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, polisi wameingilia kati kwa vile ndoa hiyo ilihusu msichana wa miaka 17 na aliyekatishwa masomo yake kuolewa na bwana wa umri wa miaka 50.

Polisi waliingia mahali hapo wakati Bi. Harusi, ndugu na waengine walioudhuria walipokuwa... soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
 
©Maggid | Date:30.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 14
Utamu Wa Chungwa.....


Hausimuliwi kwa kula nanasi! Huu ni msimu wa machungwa, na yapo bwelele, chungwa moja linaanzia shilingi hamsini. Pichani ni Mtaa wa Jamhuri, Dar, jana mchana.
 
©Maggid | Date:30.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 2
Mtoni Mtongani
 
©Maggid | Date:30.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
FC Vito Malaika Ya Newala Wako Helsinki
Please inform the Tanzanian society that FC Vito Malaika from Newala plays in Helsinki Cup 2009. Matches start on 6th July. We will put all fixtures on www.liike.fi as soon as we get them from Helsinki Cup.



Karibuni wote cheer up the Malaika from South!



Br. Ari





Ari Koivu
Toiminnanjohtaja - Executive Director
LiiKe - Sport & Development

Radiokatu 20
00093 SLU, Helsinki, Finland
Telephone: +358 9 3481 2610
Fax: +358 9 3481 2602
Mobile: +358 40 765 9900
e-mail: ari.koivu@liike.fi
www.liike.fi
 
©Maggid | Date:30.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
FC Vito Malaika Ya Newala Wako Helsinki
Please inform the Tanzanian society that FC Vito Malaika from Newala plays in Helsinki Cup 2009. Matches start on 6th July. We will put all fixtures on www.liike.fi as soon as we get them from Helsinki Cup.



Karibuni wote cheer up the Malaika from South!



Br. Ari





Ari Koivu
Toiminnanjohtaja - Executive Director
LiiKe - Sport & Development

Radiokatu 20
00093 SLU, Helsinki, Finland
Telephone: +358 9 3481 2610
Fax: +358 9 3481 2602
Mobile: +358 40 765 9900
e-mail: ari.koivu@liike.fi
www.liike.fi
 
©Maggid | Date:30.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Monday, June 29, 2009
Picha Moja,Tafsiri Elfu Moja!


Ukiitazama vema picha hiyo utaona noti ya shilingi elfu kumi aliyopewa msichana huyo mwanafunzi. Hapo ni eneo la Polisi Chang'ombe,jana Jumapili( Picha:KWANZA JAMII)
 
©Maggid | Date:29.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 12
Yote Ya Mungu


Mitaa ya kati,Temeke jana Jumapili.
 
©Maggid | Date:29.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Mchumia Juani


Temeke,jana mchana.
 
©Maggid | Date:29.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
Kichina!
 
©Maggid | Date:29.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 6
Bora Mkono Huende Kinywani
 
©Maggid | Date:29.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
KWANZA JAMII Juma Hili


Soma KWANZA JAMII mitaani na mtandaoni; http://www.kwanzajamii.com
 
©Maggid | Date:29.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Sunday, June 28, 2009
Tufanyeje Ili Turidhishane Kimapenzi?


Ilibainishwa humu hivi karibuni kuwa utafiti ulionyesha kuwa baadhi ya wanaume wana haraka ya kufanya sex. Habari ile bado inawafanya baadhi yenu kuendelea kunitumia mails zenye michango ya hoja na maswali pia. Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
 
©Maggid | Date:28.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
Sheikh Suleiman Gorogosi Amefariki Dunia Jana


Kaimu Mufti Mkuu, Sheikh Suleiman Gorogosi amefariki dunia katika ajali ya gari jana akiwa safarini akitokea Mtwara kwenda Lindi. Anatazamiwa kuzikwa leo. Sheikh Gorogosi ameacha pengo kubwa kwa uongozi wa BAKWATA, Waislamu na Jamii ya Watanzania kwa ujumla wake. Mungu Amlaze Mahala Pema Peponi,AMEN.
 
©Maggid | Date:28.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
8-1: Namna Gani Bongo FC?!


Timu ya Watanzania waishio Sweden Kilimanjaro Stars iliwachabanga wenzao wa Bongo FC wa Finland kwa mabao 8-1. Ilikuwaje? Tunasubiri simulizi!
 
©Maggid | Date:28.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 3
Prof. Haroub Othman Hatunaye Tena


PROFESA HAROUB OTHMAN ( PICHANI) AMEFARIKI DUNIA. NI KWA MUJIBU Wa TAARIFA ZILIZORIPOTIWA KWENYE MICHUZI BLOG NA MWANA WA MAREHEMU, TAHIR OTHMAN. MAREHEMU ALIKUTWA AMEFARIKI ASUBUHI HII AMBAPO JANA ALILALA AKIWA BUHERI WA AFYA.
ATAKUMBUKWA KWA MCHANGO WAKE MKUBWA KWA TAIFA LETU.
 
©Maggid | Date:28.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 2
What is Development? Colonialism Deconstructed


Makala hii ya Profesa Mbele ilichapwa katika toleo la kwanza la ' KWANZA JAMII' chini ya kichwa cha habari; ' Maendeleo ni nini'. Mwandishi ameifanyia tafsiri na kuchapwa na gazeti la The Urban Fly la nchini Marekani. Tunamshukuru Profesa Mbele kwa jitihada zake za kusambaza maarifa hata yakafika Kasulu Kigoma, Marekani na kwingineko.

By Dr. Joseph Mbele
The Urban Fly
The concept of development is everywhere, in our personal lives and in the lives of communities and countries in general. We all believe that we need development. If we do not strive to develop, we get pressured in one way or another to do so. Other people try to force development on us. Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com, au http://www.theurbanfly.com
 
©Maggid | Date:28.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Saturday, June 27, 2009
Ngoma Afrika Band


Ras Makunja na Mzimu wake "The Ngoma Africa Band aka FFU,
wamejinyakulia nafasi ya pekee katika maonyesho ya mziki ya kimataifa ya "MASALA World Beat Festival, yaliyofanyika mjini Hannover,Ujerumani siku ya Jumapili ya 14-Juni-2009. Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
 
©Maggid | Date:27.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Afro-Music Live In Stockholm


Lilla Wien Bar and Restaurant Present's
Afro-Music Soukous and Rumba with:
Maestro Vumbi Dekula and Sammy Kasule.
Date:03-04 July 2009 (Friday-Saturday) from 21-01
Address:Swedenborgsgatan 20 Södra Station Pendeltåg
Welcome and dance with us "Soukous Mashariki na Kati"
 
©Maggid | Date:27.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Ghorofa La Kwanza Kinondoni Biafra!


Ni la Bwana Majaliwa, kuna mnaomkumbuka.
 
©Maggid | Date:27.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 4
Consultancy
Salaam Kaka Mjengwa

Hongera kwa kutupa habari za Bongo. Hapa tumeanzisha Firm ya Consultancy ya Biashara na taaluma, tunaomba uwahabarishe wadau kwa utambuzi. Tovuti yetu ni www.zabacco.com.

Kheri nyingi ziwe nawe

President
Zanzibar Business and Academic Consultancy
 
©Maggid | Date:27.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 2
Friday, June 26, 2009
Mwinyi" Eeh Michael,Unaionaje Tanzania Yetu?"


Rais Mstaafu Mzee Ali Hassan Mwinyi alipata kukutana na Michael Jackson alipotembelea Tanzania.
 
©Maggid | Date:26.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 3
Michael Jackson Amefariki Dunia


Akiwa na miaka 50. Michael Jackson ni legend; aliishi na kufanya mengi yaliyo mbele ya wakati wake. Atakumbukwa.

Michael Jackson aliwahi kufika Tanzania kwa ziara ya kitalii miaka ya 90. Inasimuliwa, kuwa pale Kilimanjaro Hotel alipofikia alisikia kelele za washabiki jioni ile. Akachungulia dirishani na kuuliza kama wamekuja kumwona yeye. Akajibiwa; ” Hao ni washabiki wa klabu ya Simba wanarudi wakishangilia ushindi wa timu yao wakitokea Uwanja wa Taifa na kwenda kukiwahi kivuko. Katika wakati ule ambapo televisheni hazikuwapo, Michael Jackson hakuwa maarufu sana kuizidi Simba na Yanga!
 
©Maggid | Date:26.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 3
Haya Tena!


Ni kwenye Vodacom Dar Half Marathon hivi karibuni.
 
©Maggid | Date:26.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Thursday, June 25, 2009
Picha Hii Na Maadili: BAP Anachambua Kwa Kina


“Je, ni makosa kwa mpiga picha endapo mtoto huyu ataliwa na tai?Au si kosa kwa mpiga mpicha kwani ametusaidia kufahamu ukubwa wa tatizo. Kwamba eneo hilo limekubwa na ukame na njaa kali kiasi cha mama kufa au kuondoka na kumwacha mtoto wake.”

Swali na tamko hilo hapo juu ni mojawapo ya viini muhimu vya uandishi (journalism) na usambazaji (dissemination) wa habari na mawasiliano. Yote hayo mawili yana utata wake:

Mosi, wanahabari wanakabiliwa na maswali, matatizo, na kero za ki-taaluma. Wakati mwingine huwa ni vigumu sana kuweza kueleza habari bila kuingilia kati, ingawa wataalamu wa taaluma ya habari hujigamba kuwa mwanahabari hawezi kuwa sehemu ya habari! Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
 
©Maggid | Date:25.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 6
Huduma Mpya! AIR ZARA INTERNATIONAL!


Kuanzia kesho kutakuwa na huduma mpya ya usafiri wa ndege kwa abiria ( Scheduled Commercial flights)kwenda na kutoa Zanzibar, Mafia, Iringa na kwingineko. Kwa habari zaidi tembelea; http://www.airzara.com
 
©Maggid | Date:25.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
Wanaume Waoga Wa Kutongozwa!


Baadhi ya wanaume ni waoga wa kutongozwa na wanawake. Hii ni kwa mujibu wa tafiti na uzoefu uliopo. Hapa kuna sababu za kijamii ikiwamo malezi, mila na desturi.
Bado inaonekana na wengi kama kitendo cha ajabu kwa mwanamke kuanza kuchukua hatua za kumtongoza mwanamme anayempenda ama kuvutiwa naye.Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
 
©Maggid | Date:25.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
" Nimepunguza Kidogo!"

Mmoja wa walishiriki wa Vodacom Dar Half Marathon Jumapili iliyopita.
 
©Maggid | Date:25.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
Muhogo Huu!

Mahitaji ya muhogo yameongezeka hususan katika Jiji la Dar Es Salaam na vitongoji vyake. Tafiti zaidi zinahitajika kufanywa ili kuboresha zao hili.
 
©Maggid | Date:25.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Wednesday, June 24, 2009
Changamoto Ya Kimaadili


Je, ni makosa kwa mpiga picha endapo mtoto huyu ataliwa na tai?Au si kosa kwa mpiga mpicha kwani ametusaidia kufahamu ukubwa wa tatizo.Kwamba eneo hilo limekubwa na ukame na njaa kali kiasi cha mama kufa au kuondoka na kumwacha mtoto wake. Picha hiyo iliyopigwa na mpiga picha mahiri barani Afrika ( Marehemu Mohammed Amin) ndiyo iliyouamsha ulimwengu na kutambua kuwa Ethiopia ilihitaji msaada wa haraka kutokana na kukumbwa na ukame na njaa.
 
©Maggid | Date:24.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 8
Kambona Alikuwa Na Mvuto Kwa Wanawake


Wanawake waliiga staili yake ya nywele!

Na Born Again Pagan

BADO tunajenga muktadha wa matukio ya ki-mataifa, ki-ukanda (regional) na ki-taifa (Tanzania) uliozalisha msimamo mkali wa baadhi ya wanafunzi vijana wa Mlim,anai miaka ya 1960-hadi 1970. Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
 
©Maggid | Date:24.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
Wabunge Fungeni Virago Mwende Kwenu!


Wabunge Fungeni Virago Mwende Kwenu!

Na Padri Privatus Karugendo

KATIKA hali ya kawaida hakuna Mtanzania aliyekuwa na imani kwamba Wabunge wetu wangeweza kukwamisha Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka 2009/2010; wengi tuliamini ingepitishwa kama zinavyopitishwa zote kila mwaka. Kuna sababu nyingi za kuamini hivyo: Idadi kubwa ya Wabunge ni ya chama tawala, Bajeti inaandaliwa na serikali, na !serikali inaongozwa na chama tawala: Haiwezekani chama kikajikwamisha hata kama bajeti ingekuwa mbaya namna gani. Rais wa nchi anatoka chama tawala yeye ndiye mwenyekiti wa chama hicho tawala; hotuba yake kabla ya bajeti ilikuwa inatengeneza njia; uchaguzi mkuu ni mwaka kesho, wabunge wote wa chama wanapita katika mchakato wa chama, hivyo ni lazima kuwa “watoto” wazuri ili wateuliwe kugombea tena katika uchaguzi mkuu ujao; hata hivyo hakuna historia ya Bunge la Tanzaniaa kukwamisha bajeti. Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
 
©Maggid | Date:24.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 3
Hata Kama Kutangulia Si Kufika...


Pamoja na kuongoza kundi hilo kwa kasi nzuri ya kuanzia, baada ya km 10 hivi nilimkuta kijana huyo mwenye namba 301 akitembea kama mtu anayekwenda dukani pale maeneo ya Kivukoni Front. Natumaini aliweza kumaliza km 21 hata kwa kutembea. Naam. Hata kama kutangulia si kufika, ni bora ufike salama.
 
©Maggid | Date:24.6.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
   
 
Copyright 2006 © MAGGID MJENGWA. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu