GAZETI LA UCHAMBUZI MAKINI LENYE KUIHUSU NA KUIGUSA JAMII. NI GAZETI LA KILA WIKI. LITAANZA KUONEKANA MITAANI JUMANNE, MACHI 31, 2009. USIKOSE NAKALA YAKO!
Saturday, November 21, 2009
Chalinze By Night!

Chalinze, jana mchana.
 
©Maggid | Date:21.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Kwa Mkulima: Soko Bado Chafu


Pichani ni kijijini Ruaha Mbuyuni jana asubuhi. Bei ya kitunguu kwa debe bado ni shilingi elfu tatu.
 
©Maggid | Date:21.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Ulimwengu Wa Mahaba: ( Mada Endelevu) Hiki Ndicho Kinachomsisimua Mwanamke...


Mada inaendelea… ( Maoni ya Mdau)
Wanaume wengi huelewa kuwa kuna umuhimu wa kumuandaa mwanamke kwa kumshika shika maungo yake ya mwili lakini wengi hupuuzia suala hili kwa kuwa wao hamasa yao ya mapenzi huamka na mwili husisimka tayari kwa kuanza kushiriki tendo la ndoa mara tu baada ya kuona mwili wa mwanamke ukiwa mtupu. Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
 
©Maggid | Date:21.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 2
Friday, November 20, 2009
Meshack Maganga
Halo kaka Maggid sasa nomba kutangaza blog yangu kupitia hapa kijijini kwetu
www.magangam.blogsport.com
 
©Maggid | Date:20.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 2
Rusumo.com
Pole na shughuli za kutupasha habari mbali mbali zinazotekea hapo Tanzania.
Naomba uniwekee ombi langu katika glob yako.
Nimetengeneza website www.rusumo.com ambampo wadau wataweza kusikiliza nyimbo mbali mbali za Kitanzania kama vile taarab,dance,bongo flava,segere na nyengine nyingi tu.
Pia kuna dictionary ya kisasa kabisa ambayo ina lugha zote za Asia na baadhi ya lugha za Asia.
Baada ya kupata tafsiri ya neno pia unaweza kuonesha picha zinazo husiana na neno hilo upande wa kulia wa ukurasa.
Wadau pia wanaweza kuona hali ya hewa na wakati wa sehem mbali mbali za dunia.
Ndugu wadau Karibuni sana.
Ni mimi
MSAFIRI ISMAIL RUSUMO.
msafiri@rusumo.com
 
©Maggid | Date:20.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
Nimewasili Dar Salama Mchana Huu
Nikitokea Iringa. Dar leo Ijumaa ina jua kali na joto pia. Vinginevyo, katika heka heka za jiji kubwa kama hili bado naiona Dar iliyo tulivu.
 
©Maggid | Date:20.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
UTanzania Kwanza!


Hapo kuna Mheshimiwa Mama Diwani ( CCM) kuna vijana wa CCM, CUF na CHADEMA. Vyama hivyo ni vya kisiasa tu. Watanzania tuna utamaduni wa kushirikiana kijamii bila kujali siasa, dini, rangi au kabila.Huo ndio UTanzania. Kidogo kidogo zimeanza kupandikizwa mbegu za Watanzania kuchukiana na kubaguana kwa sababu za kisiasa, kidini, rangi na kikabila. Tuna cha muhimu sana cha kuwarithisha watoto na wajukuu zetu; UTanzania Kwanza. Pichani ni Iringa, jana alhamisi.
 
©Maggid | Date:20.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 6
TEKNOHAMA
Kaka Maggid pole na kazi ya kuendeleza taifa!!

Kaka sisi ni wajasiliamali wa teknolojia ya mawasiliano ya kompyuta.

Sasa hivi hakuna haja ya kuagiza software kutoka nje ya nchi,tujivunie kilicho chetu.

Tunatengeneza software za aina mbalimbali kama Payroll, Hospital & Pharmacy System Management, Supermarket Cash System, School System Management, Dry Cleaner System software na nyinginezo nyingi tu..

Kwa mawasilano zaidi wasiliana nasi kwa email ifuatayo: pcresourcesltd@gmail.com
 
©Maggid | Date:20.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 2
Kuna Aulizaye; "Uko Wapi Profesa Matondo?
Profesa Matondo, upo wapi?

nyumba yangu
nyumba zangu

ANGALIA HII:

ng'ombe yangu
ng'ombe zangu

AU ni

ng'ombe wangu
ng'ombe wangu

NA HII PIA:

mama yangu
mama zangu

AU ni

mama wangu
mama wangu?
 
©Maggid | Date:20.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Thursday, November 19, 2009
Mambo Ya Viriyala Haya!

 
©Maggid | Date:19.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 6
KWANZA JAMII WIKI HII


Liko mitaani tangu Jumanne ya juma hili.
 
©Maggid | Date:19.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania.


Mtoto wa mtaani akiwa amechapa usingizi katika nguzo ya taa ya barabarani iliyoanguka katika barabara ya Bibi Titi Mohammed jijini Dar es Salaam bila kujali usalama wake kutokana magari kupita karibu yake.
Ahsante ya picha:Fidelis Felix
 
©Maggid | Date:19.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 3
Mheshimiwa Anne Kilango Alivyolia na Wapiga Kura Wake GohaK

Mbunge wa Same Mashariki,Anne Kilango Malecela akilia kwa uchungu juzi baada ya kufika kijiji cha Goha kulipo tokea maporomoko na kuuwa watu 24 Wilayani Same.
Asante ya picha: Haki Ngowi
 
©Maggid | Date:19.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 5
Ziara Ya Mama Kikwete Singida


Mke wa Rais Mama Salma Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo(WAMA)akiwa amebeba kibuyu mara baada ya kukabidhiwa na wanawake wa kabila la wataturu ikiwa ni ishara ya kumkaribisha katika mkoa wa Singida.Mama Kikwete yuko katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani humo.
Ahsante ya picha: Juma Kengele-Ikulu
 
©Maggid | Date:19.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
MEMORIAL SERVICE,WASHINTON DC


Tujumuike na familia ya Elias Stafford Mshana(Massawe) katika ibada jumapili november 22 saa nane mchana(2:00pm) ya kumuombea mama yao mpendwa Bertha Stafford Mshana aliyefariki nov 12/2009 katika hospitali ya KCMC,Moshi Kilimanjaro na kuzikwa november 16/2009,Moshi,Kilimanjaro

Ibada itafanyika
Good Samaritan Lutheran Church,
10110 Greenbelt Road,
Lanham,Md,20706.
Sisi tulikupenda lakini mwenyezi Mungu amekupenda zaidi,ukae katika amani mpaka hapo mwenyezi Mungu atakapo tukutanisha tena,yeye alitoa na yeye ametwaa,jina lake lihimidiwe.

Kwa maelekezo zaidi,wasiliana:
Marco Mbullu 571 426 7124 ,
Elvis Saria 301 213 0657 ,
Elias Stafford 301 646 5683
Ray Abraham 301 793 4467
 
©Maggid | Date:19.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Salim Na Ng'ombe Zake- Wanamjua Na Anawajua Kwa Majina!


Pichani ni Salim Abri 'Asas'. Ni rafiki yangu wa tangu nifike Iringa miaka mitano iliyopita. Ni kijana mfanyabiashara, mkulima na mweledi wa masuala ya kisiasa na kijamii. Jana jioni tuliongozana hadi shambani kwake. Tunapozungumzia ' Kilimo Kwanza' kuna umuhimu wa kuchota uzoefu wa wakulima kama akina Salim. Picha zaidi na maelezo nitawaletea nikipata nafasi kati ya leo na kesho.
 
©Maggid | Date:19.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 9
" Huyu Ndio Ng'ombe Wa Shughuli!"- Ng'ombe Nyati!


Kuna wakati Rais Jakaya Kikwete alitembelea maonesho ya kilimo Bulawayo, Zimbabwe, akamwona ng'ombe mkubwa. Akamtamkia mpiga picha wake; " Huyu ndio ng'ombe wa shughuli!" Kama JK angefika shambani kwa Salim Abri ' Asas' ndipo angepata jibu la Tanzania la ' ng'ombe wa shughuli!
 
©Maggid | Date:19.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
" Kiwanja Tulivu Kuliko Vyote Duniani!"- Ndege Ya Kwanza Ya Abiria Kutua Leo.



Hata kama hamjamaliza soda zenu, mnaweza kumwomba rubani awasubiri kidogo! Ni Nduli Airport, Kilomita 30 kutoka Iringa mjini njia ya kwenda Dodoma. Ndege ya kwanza ya abiria inatarajiwa kutua leo, na baada ya hapo itaelekea Mbeya na kurudi kwa kufuata route hiyo hiyo. Nauli inakaribia laki moja na themanini kwa Iringa hadi Dar. Iringa hadi Mbeya ni laki na arobaini hivi. Usafiri huo utakuwa ni kila Jumatatu na alhamisi. Ni hatua muhimu kimaendeleo.
 
©Maggid | Date:19.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 5
V.I. P Lounge: Nduli ' International' Airport!


Iringa.
 
©Maggid | Date:19.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Wednesday, November 18, 2009
Kushangilia Kosa La Jinai Mecca!



JEDDAH: Jeddah and Makkah police have arrested over 50 Egyptian nationals who were celebrating a crucial World Cup qualifying win against Algeria on Saturday. They were accused of holding up traffic and causing chaos.

Egyptian fans took the streets holding flags and celebrating, with Saudi revelers also joining in. Police acted immediately after they were inundated with complaints. The arrested was kept in police detention and released within 24 hours.

Some Egyptian fans said they did not know that celebrating was illegal in Saudi. Rabea Mahmoud, who was held in Al-Kandara police station, was surprised at being arrested when it should have been a happy occasion. “I am sad I was held but at the same time I am happy that my team renewed its hope to qualify for the World Cup. I think it was worth it despite staying in a police station for a day.”

Coffee shops in Jeddah were packed with Egyptian fans waiting for their national team’s match against fierce rivals Algeria. Some Egyptians had taken the day off, given so much was at stake. Accountant Wael Abdullah said he did not go in because he could not concentrate on work, despite the match being played late at night. He said that he had lost hope until Emad Metib scored deep into injury time in Cairo to give Egypt a 2-0 win and guarantee a play-off in Sudan.
Before the match Egyptian fans brought their drums into coffee shops and were cheering for their country
 
©Maggid | Date:18.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 5
Natabiri Misri Watashinda Na Kucheza Kombe La Dunia!


Misri wanaamini pia katika ' kafara' na mengineyo kama hapo pichani. Lakini kikubwa wanacheza Sudan, na kila nikiangalia rekodi yao ya kucheza hapo Sudan, nawaona Misri wakiwafunga Algeria na kuchukua tiketi ya kwenda Afrika Kusini mwakani.
 
©Maggid | Date:18.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 15
MSIBA : Mzee Godfrey Kyabulyo
Ndugu Andrew Kyabashasa wa Rome, Italy anasikitika kutangaza kifo cha kaka yake Mzee Godfrey Kyabulyo kilichotokea usiku wa kuamkia leo tarehe 17 November 2009 Katika Hospitali ya Mikocheni, Dar Es Salaam. Mipango ya kusafirisha mwili wa marehemu kwenda Burugo, Bukoba kwa ajili ya mazishi inafanyika Ada Estate Kinondoni nyumbani kwa binti yake Winifrida Kyabulyo.

Mungu alitoa, na Mungu ametwaa jina lake lihimidiwe.

Kwa niaba ya Watanzania hapa Roma na Italia kwa ujumla tunakupa pole. Mwenyezi Mungu amlaze Marehemu Mzee Godfrey Kyabulyo Mahali Pema Peponi. Amina


Andrew Mhella

Katibu wa Watanzania Italia Tawi la Roma

Source: www.watanzania-roma.blogspot.com
 
©Maggid | Date:18.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Mtanzania Kutalii Mbugani Ni Shilingi Elfu Moja Tu!


Ruaha National Park, Iringa.
 
©Maggid | Date:18.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 7
Tuesday, November 17, 2009
Si Udhaifu Wanaume Kuharakisha Kufanya Sex- Wana Haraka!



Tumewahi kuwa na mjadala hapa juu ya mada hiyo hapo juu. Kuna wengi wamechangia. Kwa mujibu wa maelezo ya kitaalamu, kwa mwanamme kuwa na haraka katika kufanya sex kunachangiwa kwa kiasi kikubwa na maumbile yake. Hata hivyo, ni vema mwanamme akaelewa kuwa.... Soma zaidi: http://www.kwanzajamii.com
 
©Maggid | Date:17.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 2
" Tembo Wa Tungamalenga Na Store Nyingine...!"



Salama Mwenyekiti,
Pole na majukumu ya kila siku.

Nimevutiwa sana na story yako ya Tembo wa Tungamalenga. Mimi ni mdau wa adventure safaris so hiyo story imenikumbusha baadhi ya encounters zangu na wanyama wa porini.
Hivi karibuni nimeanza kuingia ktk mtandao kwa kuwa na blog yangu (http://tembeatz.blogspot.com/) ambayo napost picha zinahosu sehemu mbali mbali nilizowahi kutembelea na kuzigandisha ktk kamera.
Mwelekeo wangu zaidi ni kwenye picha za wanyama pori na mazingira yao.

Kwa jinsi nilivyoona wadau wamevutiwa na story yako ya tembo, nitaanza kuandika na kuandaa story sambamba na picha zangu.
 
©Maggid | Date:17.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
" E Bwana We, Tumeonana Tena!"


President Jakaya Mrisho Kikwete meets the UN Secretary General Ban-ki-Moon at the FAO Headquarters in Rome during the World Summit on Food Security yesterday.
 
©Maggid | Date:17.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
"Eh, Tyson, Ya Kwetu Tunaiweka Vipi?"


President Jakaya Mrisho Kikwete in discussion with the Minister for Agriculture Stephen Wassira and Zanzibar's Minister for Agriculture,Natural Resources,environment and Cooperatives Mr.Burhani Saadat Haji at the FAO Headquarters during the plennary session of the World Summit on Food Security held in Rome yesterday(Photo: Freddy Maro).
 
©Maggid | Date:17.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
JK Na Mkurugenzi Wa Chakula Duniani


The FAO Director General Mr.Jacques Diouf escorts President Jakaya Kikwete out of his Rome office shortly after they held talks at the FAO headquarters this morning.President Kikwete is in Rome to attend the World Summit on Food Security(Photo: Freddy Maro)
 
©Maggid | Date:17.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
" Jirani Tunakutana Ugenini!"


President Jakaya Mrisho Kikwete meets Burundi President Pierre Nkurunziza in Rome shortly before the president addressed the World Summit on food Security yesterday afternoon (Photo: Freddy Maro)
 
©Maggid | Date:17.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
JK Ahutubia Mkutano Wa Dunia




President Jakaya Mrisho Kikwete delivers his speech during The World Summit on Food Security at FAO Headquarters in Rome yesterday ( Photo: Freddy Maro)
 
©Maggid | Date:17.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
KWANZA JAMII: Taifa Katika Fedheha


Taifa katika fedheha

*Siasa zisizo na tija zaharibu haiba ya nchi
*Misuguano ya chama tawala yazua hofu
*Udhaifu wa wapinzani waacha ombwe
*Mdudu CHADEMA mkono wa kigogo?
*Halmashauri Kuu yasubiriwa kukata ngebe


Na Mwandishi Wetu

KURUSHIANA maneno ya hasira, chuki na visasi vya wanasiasa wenye mvuto na ushawishi ndani ya chama tawala – Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumeiweka nchi katika fedheha kubwa.

Suala la kufikia hata waliokuwa viongozi waandamizi ndani ya chama au Serikali, kwa nafasi kama za Waziri Mkuu au za uwaziri na sasa kuirudi Serikali, chama au viongozi wenzao, ni mpasuko ambao usipoangaliwa utaendeleza fedheha hadi nchi kukosa sifa machoni mwa wawekezaji na wahisani. Soma zaidi; http://www.kwanzajamii.com
 
©Maggid | Date:17.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Mkutano: Watanzania Japani

Mkutano wa Jumuiya ya Watanzania Japani.

Uongozi wa Jumuiya ya Watanzania waishio nchini Japani (Tanzanite society) unapenda kuwaarifu
kuwa, kutakuwa na mkutano mkuu wa mwisho wa mwaka wa Wanajumuiya wote utakaofanyika:
Tarehe: 6/12/2009
Mahali(Ukumbi) : odasaga plaza (Odakyu sagamihara station)
Muda: Kuanzia saa 12:15 jioni

Agenda za mkutano huu ni kama zifuatazo:
(1)Kupata taarifa mbalimbali za maendeleo ya Jumuiya. (i.e Kuisajili Jumuiya kuwa NGO)
(2)Kujadili na kutathmini zoezi la ulipaji ada za kila mwezi.
(3)Kujadili na kuamua kuhusu kutenga fedha kwa ajili kusaidia wenye shida nyumbani Tanzania.
(4)Mengineyo.

Uongozi unapenda kuchukuwa fursa hii kuwakumbusha wanajumiya kuwa, kama tulivyokubaliana katika
mkutano uliopita, kwa wale wote watakaochelewa kufika kwenye mkutano au wasiofika bila kutoa taarifa
rasmi kwa uongozi watatozwa faini.

Mkutano utaanza rasmi saa 12:15 jioni, tunaomba kuzingatia muda.

Taarifa za kutoweza kufika kwenye mkutano zipelekwe kwa Katibu Mkuu wa Jumuiya Bw Julluis Mwombwki :
Simu: 09041304754
Email ya simu:jullius57@ docomo.ne.jp
Email:jlmwombekijnr@gmail.com

(NB) Ili kudhibiti nidhamu kwenye mkutano huu, wale wote wasio wanachama(Wanajumui ya)
hawataruhusiwa kuingia kwenye chumba cha mkutano.

Ahsanteni
Uongozi, Jumuiya ya Watanzania Wanaoishi Japani( Tanzanite Society)
 
©Maggid | Date:17.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 3
Monday, November 16, 2009
Simba ' Taifa Kubwa!'


Tumemaliza mechi zote kumi na moja za raundi ya kwanza kwa kushinda mechi zote! Simba tuko vizuri na tuna mpango mkubwa. Tunataka kucheza fainali ya Kombe la Mabingwa Afrika. Tutaandika historia. Poleni sana watani zetu!
 
©Maggid | Date:16.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 2
Novemba Ndio Hii, Lakini...



Nasikitika safari yangu ya baiskeli kutoka Iringa kwenda Dodoma kupitia Great North Road nimelazimika kuisogeza mbele. Kuna ugeni kutoka Chuo Kikuu Cha Linkoping cha nchini Sweden unaotarajiwa kuwasili nchini juma lijalo. Uwepo wangu unahitajika. Vinginevyo, maandalizi ya safari nilishayakamilisha. Nitaangalia upya kalenda yangu na bila shaka mapema mwakani nitaweza kuifanya safari hiyo kama kila kitu kitakwenda sawa.
 
©Maggid | Date:16.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 3
Kumekucha!


Kijijini Tungamalenga, Iringa.
 
©Maggid | Date:16.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
Sunday, November 15, 2009
Tafakuri Jadidi Ya Juma Hili: Nani Atamsaidia Mtoto Wa Kike Kijijini?


Pichani ni kijijini Tungamalenga, Idodi, Iringa. Picha kama hiyo unaweza kuipiga katika vijiji vingi vya Tanzania. Tafakari, jadili.
 
©Maggid | Date:15.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 5
" Tunachagua!"


Kijijini Tungamalenga, Idodi, Iringa.
 
©Maggid | Date:15.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 2
Saturday, November 14, 2009
Hapa Hakuna Cha Suti Na Tai!

Rais Barack Obama akiwa na viongozi wenzake wakati wa hafla ya chakula cha join (Gala Dinner): ktoka kushoto mwa picha, Waziri Mkuu wa Japani Yukio Hatoyama, rais wa Indonesian Susilo Bambang Yudhoyono Waziri Mkuu wa Singapore Lee Hsien loong na Rais wa China Hu Jintao.
Chanzo: Associated Press (Sat Nov 14, 10:12 AM ET)
 
©Maggid | Date:14.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
JK Awafariji Waathirika Wa Mafuriko Msoga; Ahimiza Ujenzi Wa Nyumba Bora


Pichani, Rais Jakaya Kikwete akiangalia uharibifu wa majengo baada ya mvua kubwa iliyoambatana na upepo na kusababisha mafuriko. ( Picha: Freddy Maro)

JK atembelea waathirika wa mafuriko Msoga: Ahimiza ujenzi wa nyumba bora

Na Freddy Maro
Msoga
14 Novemba 1009.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete ametoa wito kwa wananchi maeneo ya vijijini kujenga nyumba bora kwa njia ya ushirikiano na kwa kutumia teknolojia rahisi hususan matofali ya kuchoma na yale yasiyotumia saruji ili kuepuka madhara yanayoletwa na majanga ya asili kama mvua kubwa zinazoambatana na upepo mkali.

Rais Kikwete ametoa wito huo leo wakati alipowatembelea baadhi ya wakazi wa kijiji cha Msoga,wilayani Bagamoyo ambao baadhi ya nyumba zao zimeharibiwa vibaya na mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali iliyonyesha kijijini hapo hivi karibuni.

“Nimetembelea baadhi ya ya maeneo yaliyokumbwa na tatizo hili na nawapa pole kwa uharibifu mkubwa wa nyumba na upotevu wa mali uliotokea na ningependa kutoa wito kuwa tujenge nyumba bora kwa kutumia teknolojia rahisi na kwa kushirikiana kujenga nyumba moja baada ya nyingine,” alisisitiza Rais Kikwete.

Rais Kikwete alisema tayari amekwisha nunua mashine ya kutengenezea matofali yasiyotumia saruji na kwamba kwa kutumia wataalamu wa shirika la umoja wa mataifa la UN Habitat wananchi wa Msoga watanufaika na mradi wa ujenzi wa nyumba bora kwa gharama nafuu.

Akitoa taarifa ya janga hili mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Magesa Mulongo alisema kuwa thamani ya uharibifu katika nyumba ni jumla ya shilingi 10,024,688/= na kuwa nyumba zilizoathirika ni za wenyeji pamoja na jengo la muda la wakandarasi wa kichina wanaojenga majengo ya shule mpya ya msingi,nyumba ya muuguzi wa zahanati,darasa moja la shule ya msingi.

Kuhusu hatua zilizochukuliwa na serikali kukabili janga hilo, Mkuu huyo wa wilaya amesema kuwa timu ya wataalamu imeshatayarisha taarifa ya tathmini ya uharibifu na kuwa uongozi wa wilaya umepeleka msaada wa awali wa tani moja ya unga kwa waathirika na kuwa mwanzoni mwa wiki ijayo tani nne za mahindi zitapelekwa.

“Wataalamu wa afya na ustawi wa jamii watakwenda kijijini kuona maendeleo ya waathirika na pia kujua mahitaji yao kwa sasa, ,”alisema bwana Mulongo na kuongeza kuwa uongozi wa wilaya unawasiliana na wadau mbalimbali kwa ajili ya misaada zaidi.
 
©Maggid | Date:14.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 1
"Eh Mzee Wangu Ilikuwaje?"


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimfariji Mzee Philipo Pagali mkazi wa kijiji cha Msoga wilayani Bagamoyo ambaye nyumba yake aliyokuwa anaishi iliharibiwa vibaya na upepo mkali ulioambatana na mvua kubwa iliyonyesha hivi karibuni.Jumla ya nyumba 51 ziliezuliwa paa zake na kusababisha watu zaidi ya 190 kukosa mahali pa kukaa na kulazimika kuhifadhiwa na majirani(Picha: Freddy Maro)
 
©Maggid | Date:14.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Siku Nilipoifuata Njia Ya Tembo Wa Tungamalenga






Wakati mwingine tunajikuta tumo katika hatari ya kimaisha. Ndio maisha. Ijumaa ya tarehe 6 ya mwezi huu wa Novemba nililala kijijini Tungamalenga, Idodi, Iringa. Tunaweza kabisa kusema kuwa, si tu kijiji hiki kinapakana na mbuga ya Wanyama ya Ruaha bali kimo ndani ya mbuga hiyo kutokana na mazingira yake yalivyo na hususan jinsi wanyama walivyo karibu kabisa na kijiji hicho.

Jioni ile ya Ijumaa ya juma la jana nikiwa na kamera yangu begani niliamua kuzunguka kijijini na kuongea na baadhi ya wanakijiji. Hivi ni nini kero kubwa ya kijiji hiki? Nilimwuliza kijana Hussein Abdalah, fundi Seremala na mkulima kijijini. Hussein ambaye hakusita kuniambia kuwa hukata ' kiharamu' miti ya mbao ndani ya mbuga ya Ruaha alionekana kuwa mwenye taarifa na maarifa mengi katika mazingira wanamoishi.
" Braza sisi hapa kijijini hatuna ugomvi na simba, tuna ugomvi mkubwa na tembo na wanalindwa na Serikali. Ukimwua tembo mmoja ni faini ni zaidi ya milioni tano. Kwa kifupi tembo hasa wakati huu wa kiangazi na ukame wanaingia kwa makundi kwenye mashamba yetu. Wakiingia shambani kwako wanafyeka kila kitu kwa maana ya kula. Wanakula matikiti, nyanya, mahindi, mpunga, yaani hawa jamaa zetu hawaachi kitu shambani. Sasa tikitoa taarifa kwa watu wa TANAPA tunaambiwa fidia ya Serikali ni laki moja kwa eka! Na bado mkulima anaambulia elfu ishirini tu kwa eka, nyingine jamaa wanatia mfukoni." Kijana Hussein alinisimulia kwa masikitiko.

Nilimwuliza tena; " Tatizo ni tembo tu?" Akanijibu.

" Ndio hivyo braza, ugomvi wetu sisi ni tembo tu, kama itatokea vita hapa, basi itakuwa ni vita kati yetu na tembo. Simba hatuna matatizo nao hata kidogo. Wanakuja kijijini mara kwa mara. Lakini huwezi kusikia simba kamtafuna mbuzi au ndama. Wakija shida yao ni maji ya kunywa tu."

Kijana Hussein akawa tayari kunipeleka pori la jirani hapo kijijini nijionee mwenye njia wanayopita tembo na hasa muda huo wa jioni wakati giza likikaribia. Ilishatimu saa kumi na mbili na nusu jioni. Hussein na mimi tukaanza kuliingia pori kwa miguu. Wahenga walinena; " Usivamie pori kwa wembe!'. Mimi hata wembe sikuwa nao, nilibeba kamera tu! Hussein naye hakuchukua chochote. Hussein aliniambia hatutakwenda umbali mrefu porini kabla hatujaona miguu ya tembo na mavi yao. Kumbe, tuliingia porini zaidi ya nusu kilomita tukifuata njia ya tembo. Niliona miguu na mavi ya tembo, mengine yalikuwa ni ya jioni ya jana yake, bado yana ubichi. Na ghafla ndipo nikasikia mlio wa ' tarumbeta' za tembo. Nikamwambia Hussein tugeuze turudi.
" Hapana braza, wanaokuja mbele yetu ni tembo wasiozidi kumi. Wamevuta harufu yetu. Ni kutokana na upepo. Tunachotakiwa kufanya ni kuingia zaidi porini upande wa magharibi. Tuzunguke nyuma yao. Vnginevyo, wana kasi, watatufikia kabla hatujafika kijijini." Nilifahamu pia, silaha kubwa tuliyokuwa nayo ni mikono yetu. Tembo akikukaribia unachotakiwa ni kupiga makofi kama unamshangilia, naye atakimbia. Lakini hutakiwi kupiga kelele ya mdogo au kupiga honi kama umo garini. Mlio wa honi unafanana na mlio wa ' tarumbeta' ambao tembo hutoa. Tembo akisikia mlio wa honi huhisi kuna tembo mwingine aliyeingia katika ' domain' yao, ni adui. Hapo tembo anaweza kukupondaponda na kukuzika ardhini hata kama bado uko hai.

Katika hali hiyo nilifahamu, kuwa sikutakiwa kuwa mbishi bali ni kufuata maelekezo ya Hussein aliye na uzoefu zaidi wa pori lile la Tungamalenga. Tukachota zaidi pori kufuata mwelekeo wa magharibi. Ikanijia hofu kuwa tunafanyaje tukikutana na kundi la simba. Hata kama naweza kuparamia mti wa karibu lakini simba wa Ruaha wanafahamika kwa uwezo wao wa kuparamia miti. Nilihisi kifo hakiko mbali sana. Nilimwuliza Hussein wa sauti ya chini;
" Vipi tukikutana na ' masharubu'?" Simba haitwi simba porini.

" Sharubu hana tatizo. Ikitokea cha kufanya ni kutulia tu na kupita mbali naye huku tukimwangalia. " Nikafikiri kuhusu nyati pia. Lakini najua kuwa nyati walio kundini hawana tatizo, tatizo ni nyati aliye peke yake. Na kama atanikimbiza, cha kufanya ni kukimbia na kisha kuanguka kifudifudi na ' kujifanya' nimekufa. Ataishia kunilamba nguo zangu, anaweza kuzichana na labda kunichubua na ulimi wake. Mwisho nyati ataniacha kama nilivyo. Inahitaji 'kumeza barafu tumboni'. Utulie baridi na kupumua kwa mbali.

Kwa mbali tuliona vumbi likimtimka kutufuata. Iliashiria kundi lile la tembo lilishatupita. Nasi, tuliweza kulifuata nyuma kurudi kijijini Tungamalenga. Nyuma kabisa katika kundi lile la tembo kulikuwa na 'tembo mzee'. Alitembea polepole, hata kama tungekuwa nyuma ya tembo wale kwa mita kumi bado wasingepata harufu yetu. Ndio asili ilivyo. TAHADHARI: Usijaribu kutembea kwenye pori lenye wanyama wenye kudhuru kama huna mwenyeji wa eneo hilo, na zaidi uwe na maarifa ya msingi ya kukabiliana na hatari ya porini.
 
©Maggid | Date:14.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 15
Wooow! Mama Yetu Kumbe Wamo!


Pichani Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dr. Asha- Rose Migiro akionyesha sanaa ya kuicheza kandanda akiwa na Balozi wa kupambana na Malaria, Charles Ssali wa Uganda. Ssali ana umri wa miaka kumi na mbili. Anawahamasisha wenzake kwamba hawataweza kuwa mabingwa wa kandanda kama watakuwa wanasumbuliwa na Malaria. Kwa hiyo watoto, vijana, watu wazima tuungane kupambana na Malaria. Pamoja na kutumia dawa, vyandarua vyenye viatilifu ni kinga thabiti ya Malaria. ( Picha kwa Hisani ya Umoja wa Mataifa)
 
©Maggid | Date:14.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 3
Friday, November 13, 2009
" Mwenyekiti Watangazie Wanakijiji Krismasi Ya Mwaka Huu Hainikutii Dar!"


Juzi usiku nilikutana na kuongea na mwenzetu Kamala Lutatinisibwa pale Kijiweni Lumumba. Amesisitiza msimamo wake wa kuhama Dar es Salaam na kwenda kuishi Mwanza au Bukoba. Ameniambia hata nyumbani anakoishi Dar hana fenicha maana siku yeyote ile ataingia kwenye basi na kuliacha jiji.
 
©Maggid | Date:13.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 6
Nawapenda, Wananipenda!


Dada zangu wa Mtaa wa Jamhuri, Dar. Irene na Mama Imma.
 
©Maggid | Date:13.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 5
Msamvu


Morogoro, jana asubuhi.
 
©Maggid | Date:13.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Habari Ni Nyingi!


Chagga Street, Dar juzi jioni.
 
©Maggid | Date:13.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Thursday, November 12, 2009
Dodo La Mdondo!

Morogoro, leo asubuhi.
 
©Maggid | Date:12.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 4
Shida Za Njiani

Leo asubuhi. KM 30 kuufikia mpaka wa Moro na Iringa.
 
©Maggid | Date:12.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 0
Hiki Ndio Kimbembe !





Nimeondoka Dar saa kumi na nusu alfajiri ya leo. Kilomita 30 kutoka mpakani mwa Iringa na Morogoro nimekutana na shughuli hii pevu. Kifusi kimeteremshwa na mvua na kuziba barabara. Msongamano wa magari ni wa zaidi ya kilomita tano. Mengi ni malori na mabasi. Ilibidi nitumie ' ujanja wa porini' na kubahatisha kuvuka eneo hili salama. Nimewasili Iringa Mjini alasiri hii.
 
©Maggid | Date:12.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 3
Wednesday, November 11, 2009
Mazungumzo Na Rais Wa Chama Cha Walimu Tanzania




Bwaana Gratian Mkoba. Ofisini kwake Makao Makuu ya Chama hicho leo mchana. Mazungumzo yalihusu masuala ya ushirikiano hususan katika eneo la mafunzo kwa walimu. Bi. Gunnel lifstead kutoka Sweden ni Mjumbe wa Bodi ya Chama cha Walimu nchini Sweden na aliwahi kuwa Makamu wa Rais wa chama hicho cha walimu cha nchini Sweden.
 
©Maggid | Date:11.11.09 | Permalink| | Send To Your Friend | Comment: 3
   
 
Copyright 2006 © MAGGID MJENGWA. All Rights Reserved
 
Idadi ya watu